Wednesday, February 5, 2014

MCHUNGAJI AMBAKA MWANAYE


 INASIKITISHA SANA




 Na Christopher Lissa

Hakika Dunia inaelekea ukingoni. Mwanaume mmoja ambaye  aliyefahamika kwa jina la  Atanasi  Kimani mkazi wa eneo la Mbondole Kivule, Ilala jijini Dar es Salaam anayedaiwa alikuwa ni mchungaji wa kanisa la Evangelical Assemblies of God (EAGT) huko Dodoma, anashiliwa na Jeshi la Polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam kwa tuhuma za kuishi kinyumba na binti yake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 16(jina linahifadhiwa).
Habari za uhakika ambazo zimefuatiliwa kwa kina  na Sani zimetonya kuwa, Atanasi alianza kumuingilia binti yake tokea akiwa darasa la tatu ambapo sasa binti huyo yuko darasa la saba.
Baada ya kupata taarifa hizo Sani lilifika nyumbani kwa Mzee Atanasi na kuongea na mkewe, binti aliyekuwa akifanyiwa unyama huona majirani ambao walielezea kulaani vikali uchafu wa Atanasi.
Akisimulia jinsi tukio hilo lilivyobumburuka, mke wa Atanasi  Bi. Tumaini Kabeja alisema kuwa  binti aliamua kuanika ukweli  siku ya Januari 21 mwaka huu baada ya kuingiliwa na baba yake alfajiri.
"Nimeishi na mzee Atanasi kwa muda wa miaka miwili sasa pamoja na binti huyu. Huyu binti ni mtoto wa mke mwingine ambaye waliachana. Mimi ni mama yake wa kambo.Hata hivyo nilikuwa sijui lolote linaloendelea baina yao ndani, kwa sababu binti ni mdogo.Kumbe mume wangu ameanza kumwingilia mwanaye miaka mingi iliyopita na alikuwa akimtishia kuwa akitoa siri atamuuwa"alisema Bi, Kabeja.
Bi. Kabeja alisema  kabla ya kumuoa Atanasi alikuwa akiishi na watoto wake wawili binti aliyekuwa anabakwa na mwingine wa kiume lakini alimtimua mtoto wake wa kiume ili aweze kupata nafasi ya kuvuruga amri ya sita na binti yake.
"Baada ya kunioa mimi nasikia aliacha kutembea na mwanaye.Lakini alikuwa na wivu mno. Hakutaka binti atoke. Alikuwa akipmiga sana. Nilikuwa sijui kwanini? Kumbe alikuwa amemfanya mke mwenzangu. Masikini!" alisema Bi. Kabeja kwa masikitiko.
Aliongeza "Siku ya tukio, yaani Januari 21,mimi huwa nafanya bishara ya kuuza kachori shule ya msingi Mbondole, kumbe kila nikiondoka alfajiri baba mtu humfuata binti yake sebureni na kumuingilia hadi anaporidhika. Siku hiyo binti alipata maumivu sana ilibidi aniambie tu kuwa eti ni mwambie baba yake aache tabia chafu ya kumbaka. Nilishituka sana. Nilimhoji ndipo aliponisimulia kila kitu.
Siku hiyo hiyo nilimpeleka Polisi Staki Shari kutoa taarifa na tukaelekea  Hosipitali ya Amana.Nilikutana na watu wa Ustawi wa Jamii  baada ya kujiridhisha na maelezo yangu na ya mtoto  tukafanya mtego wa  kumnasa mtuhumiwa ambapo mimi nilijifanya nimelazwa hapo baada ya kuzidiwa. Alikuja mtuhumiwa akakamatwa na baada ya kumbana sana alikili kulala na mwanae ingawa alisema mara moja tu" alisimulia Bi. Kabeja na kwamba mumewe alikuwa ni mchungaji wakati akiishi Dodoma na nimaarufu kwa jina la mchungaji hadi sasa.
Sani liliweza kuongea na binti aliyekuwa akifanyiwa ukatili huo ambaye alikiri kuanza kulala na baba yake tokea akiwa darasa la tatu.
"Sijawahi kulala na mwanaume mwingine isipokuwa baba. Tokea baba alipoachana na mama kule Dodoma alituchukua mimi na kaka. Tukawa tunaishi Mbagala. Alipanga chumba kimoja na Sebure. Usiku alikuwa akitaka niwe na lala naye na kaka anabaki Sebureni. Alikuwa ananifanyia mambo ya ajabu sana. Alikuwa akiniziba mdomo  ili nisipige kelele. Nilikuwa nasikia maumivu makali mno lakini alikuwa akinitishia kuwa nisema ataniuwa"alisimulia binti huyo.
Alisema" Aliendelea kulala na baba yake hadi walipohamia eneo la Mbondole, hapo baba yake alimfukuza  mtoto wake wa kiume ili apete nafasi ya kulala naye, hadi alipomuoa Bi. Kabeja. Alisitisha kidogo kulala na mimi baada ya kuoa. Alianza tena kulala na mimi baada ya mama kupata uja uzito. Kuna kipindi alikuwa akiniingilia nyuma.Hadi Januari 21 ambapo nilichoka na kuamua kumueleza mama. Nilikuwa naogopa kwa sababu baba ni mkali sana.Huwa anatupiga sana mimi na mama na kutishia kutuuwa kwa panga"
Binti huyo alisema kutokana na kutumika sana kimapenzi na baba yake hivi sasa yuko sugu licha ya kuwa naumri mdogo.
"Naiomba Serikali iingilie kati kulishughulikia suala hili, maana baba akiachiwa atatuchinja mimi na baba.Niko darasa la saba hivyo nahitaji kusoma na kufauri ili niweze kutimiza malengo yangu"alisema Binti huyo kwa uchungu.
Mjumbe wa shina namba 25 katika eneo hilo Cosmas  Manyota alithibitisha kupokea taarifa za tukio hilo la kusikitisha na kwamba sheria lazima ichukue mkondo wake.
"Huyu jamaa kwanza muda wote yeye ni mtu wa hasira. Hana uhusiano  mzuri na wenzake. Yeye ni panga mkononi. Watoto na mkewe alikuwa anawapiga vibaya mno"alisema Manyota.
Familia hiyo imeomba msaada wa hali na mali kwa wasamalia wema kutokana na kuishi maisha magumu baada ya baba yao kutiwa mbaroni.
"Yeye ndiye alikuwa mtafutaji, lakini kutokana na unyama aliokuwa ameufanya tuliona ni vema tuteseke tu yeye aende ndani. Hatuna kitu hapa. Tunakula kwa taabu sana. Mwanangu huyu aliyekuwa anabakwa yuko darasa la saba. Anajiandaa na mitihani. Tunaomba msaada kwa watanzania wenzetu. Hata hivyo mimi najitahidi kuuza kachori lakini haikidhi mahitaji.Tusaidieni"alisema Bi. Kabeja na kwamba mtu yoyote anayehitaji kuisaidia familia hiyo awasiliane nayo kwa namba 0756701134 au awasiliane na mwandishi wa habari hizi kwa namba 0654 586788 ama afike ofisi za gazeti hili mtaa wa Shauri Moyo na Lindi Ilala Jijini Dar es Salaa au awasiliene na mtangazaji wa kipindi cha hatua Tatu cha Redio Times FM Edson Mkisi Junior  kwa namba 0718377080. Shime  Watanzania  kutoa kwako ni kuchangia jitihada za kupinga ukatili wa kijinsia kwa watoto.



 BINTI ALIYEKUWA AKIBAKWA NA BABA

No comments:

Post a Comment