Sunday, January 26, 2014

 AMAN JAPHET NGUKU  MTUNZI WA KITABU CHA SAFARI YA NDOTO AKIHUTUBIA WAKATI WA UZINDUZI WA KITABU HICHO  KATIKA UKUMBI WA BEIJING JIJINI DAR ES SALAAM



HII NDIYO  TAARIFA  FUPI YA UZINDUZI
Vijana wa kitanzania wameaswa kuacha kulalamika na kuishi katika maisha ya nadharia, badalayake  wameshauriwa  kubadilika  kuwa watendaji  na wenye uthubutu wa kutimiza malengo yao.

Hayo yamesemwa na   Mkurugenzi wa Mtendaji wa  Amajat Investment Bw. Aman Nguku  katika uzinduzi wa kitabu chake  kiitwacho SAFARI YA NDOTO kinachobeba   kaulimbiu "Siyo Serikali ni Mimi, Wewe naSisi"
Akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam, Bw. Nguku alisema, imefika wakati  sasawatanzania hasahasa  kundi la vijana  waamke  kutoka usingizini  na kutimiza malengo ya kimaisha  ambayo wanapenda kufikia.
"Imetosha sasa kusema kesho, kufikiri  bila kutenda  na kuongea bila vitendo .Kinachotakiwa nikuanza utendaji" alinukuu Bw. Nguku  kutoka katika kitabu  chake  chenye kurasa 108.
Akieleza  madhumuni ya kuandika kitabu hicho, Bw. Nguku  ambaye pia ni  mwanafunzi wa mwakawatatu  anayesomea shahada  yaUchumi  katika  Chuo Kikuu  cha Ardhi  jijini Dar es Salaam  alisema:
"Hiki kitabu ni mahususi kwa wale  watu ambao  wana ndoto mbalimbali katika maishayao lakini hawajui pakuanzia.Iwe ndoto  ya kufanyabiashara maarufu , mwanasiasa  au daktari  bingwa.Hiki kitabu ni ramani kwako"
Aliendelea kusema"Kitabu hiki kinaweza pia kuwa changamoto kwa wale  ambao wamekata tamaa katika maisha.Kwa kusoma  maandishi ya kitabu hiki, wanaweza  wakafufua  ndoto zao na kufanikiwa katika yale waliyoyapanga"
Safari ya Ndoto  pia  inabeba  dondoo kutoka kwa Baba wa Taifa  Mwalimu Julius  Nyerere, mfanyabishara maarufu Bw. Reginald mengi na Mkurugenzi wa Helvetic SolarContractors Bw. Patroick Ngowi.
Kitabu hiki kinasambazwa katika maduka  mbalimbali jijini Dar es Salaamna nchi nzima  ili watanzania wengi  wapate kukisoma. Kinauzwa kwa Tsh.5000 tu
Kwa sas, mtunzi pia anaandika vitabu vingine  viwili vyenye vichwa  'Ndogo lakinimuhimu,kesho' na What is Life for (Maisha  ni ya nini)
Kwa mawasiliano na mtunzi 
Aman Japhet  Nguku o713818409.

No comments:

Post a Comment